Vikosi
vya usalama Kananga vimekabiliana na wapiganaji wanaotaka kulipiza kisasi
mauaji ya kiongozi wao aliyeuawa na jeshi mwezi Agosti, maafisa na vyombo vya
habari vinasema.
Wanamgambo
hao waliushambulia uwanja w
a ndege wa mji huo Ijumaa na kumuua mfanyakazi mmoja
wa ndege, walioshuhudia wanasema.
Congo
imekabiliwa na ghasia za miaka kadhaa na ukosefu wa utulivu kisiasa.
Maandaamano
dhidi ya rais Joseph Kabila katika mji mkuu Kinshasa mapema wiki hii
yamesababisha vifo vya watu 50, Umoja wa mataifa unasema.
Ripoti
zinaarifu kuwa wapiganaji wanaomtii kiongozi wa kikabila aliyeuawa, Kamwina
Nsapu, waliingia katika mji wa Kananga Alhamisi asubuhi.
Kituo
cha Redio Okapi kinasema wanamgabo hao wamepambana na vikosi vya usalama na
hatimaye walitimuliwa.
Walirudi
Ijumaa na kukivamia kituo hicho cha ndege.
"Kulikuwa
na mapigano makali yaliohusisha silaha ndogo na kubwa," anasema Killy
Ilunga, aliyeuona mwili wa mfanyakazi wa ndege baada ya kuuawa.
"Waliingia
katika ukumbi wa uwanja wa ndege. Mmoja wao alimpiga kwa rungu."
Idadi
ya waliouawa haijathibitishwa, lakini ripoti zinasema idadi huenda ikawa kati
ya watu 10 na 13.
Msemaji
wa serikali Lambert Mende anasema hali imedhibitiwa.
Related Posts
RAISI MAGUFURI AJARIBIWA AMTUPA LUPANGO MHADHIRI CHUO KIKUU
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Mkwawa (Muce), Dk Oscar Magava (48). Dk M[...]
Sep 24, 2016JAKAYA MRISHO KIKWETE AZIDI KUNG'ARA KIMATAIFA
Shirika lisilo la Kiserikali laSpeak Up for Afrika &nb[...]
Sep 24, 2016MADEREVA WA MALORI WALIOTEKWA NYARA KONGO WAOKOLEWA NA VIKOSI VYA JESHI
Madereva wa malori kutoka Tanzania waliokuwa wametekwa katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya[...]
Sep 16, 2016MALORI 12 YAMETEKWA NA MADEREVA WAMETEKWA DRC KONGO
Serikali imepokea taarifa za kutekwa kwa malori 12 katika eneo la Namoyo Jimbo la Kivu Ku[...]
Sep 15, 2016MUGABE MPAKA ANYOSHE MIKONO JUU HALI YA ZIMBABWE KIUCHUMI NI MBAYA ACHUKUA HATUA MBAYA
Patrick Chinamasa Waziri wa fedha wa Zimbabwe ametangaza kwamba serikali itafuta ajira 25,000 kat[...]
Sep 09, 2016CUF WAJIBU BAADA YA LIPUMBA KUTANGAZWA KUWA MWENYEKITI
Baada ya kupokea Ushauri huo, The Civic United Front (CUF – Chama Cha Wananchi) kinapenda kueleza[...]
Sep 24, 2016LIPUMBA APEWA WENYEKITI CUF
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema kuwa Prof. Ibrahim Lipumba bado[...]
Sep 24, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.