0
Madiwani wa chama cha CUF waliofanya vurugu kwenye uchaguzi wa Umeya katika Manispaa ya jijini Tanga ambao idadi yao ni
madiwani kumi


Kamanda Zubery Mwombeji alisema “kuwa madiwani hao walikamatwa na kupelekwa katika kituo cha Polisi cha Chumbageni na baadaye waliachiwa kwa dhamana majira ya saa sita usiku.

madiwani hao walikamatwa kwa tuhuma za kufanya vurugu na kuchoma pazia na kujaribu kuvunja mlango wa ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo.”

Madiwani wa CUF wanadaiwa kufanya vurugu katika ukumbi wa halmashauri ya jiji hilo uliotumika kupigia kura baada ya Mkurugenzi wa jiji hilo kumtangaza diwani wa CCM, Mohamed Mustafa kuwa mshindi kwa kupata kura 19 dhidi ya mgombea wa CUF aliyepata kura 18.

CUF walipinga matokeo hayo na kudai kuwa walihujumiwa na kuporwa ushindi hususan kwa kuwa wana idadi ya madiwani 20 dhidi ya madiwani 17 wa CCM.

        Mimi nadhani cha msingi wangeangalia wenyewe wote ni wasafi Madiwani wao au wapo waliokura rushwa.

Post a Comment

 
Top