Mbunge wa Sikonge (CCM), Said Nkumba ambaye alihamia Chadema hivi karibuni ameamua kurejea katika chama chake cha zamani kwa madai alikosea njia.
Nkumba ambaye alihamia Chadema baada ya kushindwa katika kura za maoni kugombea ubunge Sikonge, aliteuliwa kugombea ubunge kwa tiketi ya Chadema lakini wanachama wa chama hicho walipinga kitendo cha Kamati Kuu ya chama hicho cha upinzani kumteua wakitaka mgombea wao, Hijja Ramadhan arudishwe jambo lililofanya Nkumba kuondolewa na kukosa nafasi ya kugombea ubunge.
Nkumba alipojitoa CCM alisema alikipenda kwa dhati chama hicho lakini hakuona sababu ya kuendelea kubaki kwa kuwa hasikilizwi na hakina mapenzi na watu.
Lakini akizungumza Dar es Salaam jana, Nkumba alisema amerudi nyumbani kwa kuwa alipotea njia na hakuona kama kuna mwelekeo Chadema.
Alipoulizwa kuhusu kupewa jimbo na Chadema alisema hayo yaachwe, amerudi nyumbani kwa kuwa ni kama rebound katika mchezo wa kikapu na watu wanaendelea kucheza.
Katibu wa CCM Wilaya ya Sikonge, Seleman Majilanga alisema hakuna tatizo kwa Nkumba kurejea ilimradi afuate taratibu.
. “Unajua ukishahama chama, kadi yako inakuwa haina kazi na inabidi uanze upya na yeye inabidi aende kwenye tawi lake,” alisema.
Majilanga alisema hana tatizo kumpokea mwanachama mpya au anayerudi na hajawahi kuzungumza na Nkumba kuhusiana na mchakato wa uchaguzi ndani ya chama katika kura za maoni.
“Sisi tumejipanga kufanya kampeni zetu na kushinda bila yeye na kwa uhakika ushindi ni mkubwa katika jimbo letu,” alisema.
Related Posts
NCHI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO VITA YA WENYEWE KWA WENYEWE IMEZUKA KANANGA
Ghasia za siku mbili katika mji wa Jamhuri ya kidemorasi ya Congo zimesababisha vifo vya watu 10.[...]
Sep 24, 2016CUF WAJIBU BAADA YA LIPUMBA KUTANGAZWA KUWA MWENYEKITI
Baada ya kupokea Ushauri huo, The Civic United Front (CUF – Chama Cha Wananchi) kinapenda kueleza[...]
Sep 24, 2016LIPUMBA APEWA WENYEKITI CUF
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema kuwa Prof. Ibrahim Lipumba bado[...]
Sep 24, 2016KWA USHUJAA HUU CHADEMA WANATAKIWA KUIGWA
September 19, 2016 Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA jimbo la Temeke kimemfukuza uanachama[...]
Sep 24, 2016VIONGOZI WA DINI WA WASHAMBULIA CHADEMA
Viongozi wa Dini nchini, wamesema Rais JOHN MAGUFULI Hajakataa kuzungumza wala kuwapuuza viongozi[...]
Sep 24, 2016RAISI MAGUFURI AJARIBIWA AMTUPA LUPANGO MHADHIRI CHUO KIKUU
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Mkwawa (Muce), Dk Oscar Magava (48). Dk M[...]
Sep 24, 2016JAKAYA MRISHO KIKWETE AZIDI KUNG'ARA KIMATAIFA
Shirika lisilo la Kiserikali laSpeak Up for Afrika &nb[...]
Sep 24, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.