Home
»
kitaifa
»
News
» KUGAWANYA MANISPAA YA KINONDONI MEYA WA CHADEMA APOTEZA NAFASI YAKE KUWA MEYA
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Aron Kagurumjuli amevunja
Baraza la Madiwani rasmi baada ya serikali kuigawa manispaa hiyo kuwa
mbili. Kagurumjuli alilivunja juzi saa 11:00 baada ya kumalizika kwa
Baraza la Madiwani la kawaida.
Alipokuwa
akitangaza kulivunja baraza hilo, Kagurumjuli alisema amevunja baraza
hilo kwa kuwa serikali imegawanya manispaa hiyo kuwa wilaya mbili, ya
Kinondoni na Ubungo hivyo kwa kuwa wilaya zote tayari zina wakurugenzi,
wakuu wa wilaya na makatibu tawala wa wilaya imempasa kufanya hivyo.
“Baraza la madiwani limevunjwa, kuvunjwa kwa baraza hili ni ukomo wa meya pia,” alisema.
Aliongeza kuwa wiki ijayo kutakuwa na uchaguzi wa meya katika manispaa hizo.
Meya
wa Manispaa ya Kinondoni alikuwepo kabla ya kuvunjwa kwa baraza hilo ni
Boniface Yakob ambaye amebaki nafasi yake ya udiwani.
Kuvunjwa kwa baraza hilo kulikuwa kunatarajiwa baada ya serikali kugawanya manispaa ya Kinondoni kuwa mbili.MA
Related Posts
VIONGOZI WA DINI WA WASHAMBULIA CHADEMA
Viongozi wa Dini nchini, wamesema Rais JOHN MAGUFULI Hajakataa kuzungumza wala kuwapuuza viongozi[...]
Sep 24, 2016KWA USHUJAA HUU CHADEMA WANATAKIWA KUIGWA
September 19, 2016 Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA jimbo la Temeke kimemfukuza uanachama[...]
Sep 24, 2016LIPUMBA APEWA WENYEKITI CUF
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema kuwa Prof. Ibrahim Lipumba bado[...]
Sep 24, 2016CUF WAJIBU BAADA YA LIPUMBA KUTANGAZWA KUWA MWENYEKITI
Baada ya kupokea Ushauri huo, The Civic United Front (CUF – Chama Cha Wananchi) kinapenda kueleza[...]
Sep 24, 2016BODI YA HABARI WA MWACHIA UONGOZI RAISI MAGUFURI
Bodi ya Uhuru Media Group inayosimamia vyombo vya habari vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambavy[...]
Sep 24, 2016NCHI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO VITA YA WENYEWE KWA WENYEWE IMEZUKA KANANGA
Ghasia za siku mbili katika mji wa Jamhuri ya kidemorasi ya Congo zimesababisha vifo vya watu 10.[...]
Sep 24, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.