watano
wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumdhalilisha Rais Dk. John
Magufuli na Jeshi la Polisi kutokana na mauaji ya askari polisi wanne
waliouawa na majambazi katika eneo la Mbande na Vikindu, Dar es Salaam
hi
vi karibuni.
Washtakiwa
hao walifikishwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es
Salaam mbele ya mahakimu watano tofauti na kusomewa mashtaka na Wakili
wa Serikali, Salum Mohammed.
Walisomewa
mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Emmilius Mchauru, Huruma Shahidi,
Margareth Bankika, Dk. Yohana Yongolo na Respicius Mwijage.
Akisomewa
mashtaka, mshtakiwa Dennis Mtegwa anadaiwa Agosti 24, mwaka huu eneo la
Ubungo External kupitia mtandao wa WhatsApp, aliweka maoni katika group
linaloitwa Dsm 11 4u Movement, akisema ‘JPM sijui anawaza nini
kichwani… hata samahani hajui au nilikosea hajui’, ‘nchi imefika hapa
kwa sababu ya mtu mmoja aliyeamua kujilipua ufahamu wake’, ‘sijaona
tatizo kwa hilo, ila kwa huyu bwana misimamo ambaye amesema msinijaribu
na ilhali kajaribiwa na ubwabwa wa jubilee kusema yote’.
‘Siasa
si chuki wala upinzani si uadui, ajifunze kushindana kwa hoja sio
mitutu ya bunduki na mazoezi yasiyo na kichwa wala miguu ya polisi’.
Mshtakiwa Suleiman Saidi anadaiwa Agosti 25, mwaka huu maeneo ya Kigogo, kwa kutumia mtandao wa Facebook, aliandika ‘Safi sana aisee, mi naona wangekufa kama 20 hivi halafu Simon Sirro tumuulize mazoezi wanafanyia wake zao au’.
Katika
kesi nyingine, mshtakiwa Juma Mtatuu akiwa eneo la Ocean Road, Agosti
24, mwaka huu anadaiwa kuwa alituma ujumbe katika Facebook akisema ‘Huyu
hata akifa ataenda peponi, na kufanya mazoezi kote kule wamekufa
Mbagala, mimi nitakuwa wa kwanza kuandamana kule Kahama, tarehe moja
naelekea Kahama kwa Ukuta, mimi nitakuwa namba moja kushika bendera ya
Ukuta, kifo kipo tuu, usiogope kwani mawe na mapanga yameisha’
Related Posts
VIONGOZI WA DINI WA WASHAMBULIA CHADEMA
Viongozi wa Dini nchini, wamesema Rais JOHN MAGUFULI Hajakataa kuzungumza wala kuwapuuza viongozi[...]
Sep 24, 2016KWA USHUJAA HUU CHADEMA WANATAKIWA KUIGWA
September 19, 2016 Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA jimbo la Temeke kimemfukuza uanachama[...]
Sep 24, 2016LIPUMBA APEWA WENYEKITI CUF
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema kuwa Prof. Ibrahim Lipumba bado[...]
Sep 24, 2016CUF WAJIBU BAADA YA LIPUMBA KUTANGAZWA KUWA MWENYEKITI
Baada ya kupokea Ushauri huo, The Civic United Front (CUF – Chama Cha Wananchi) kinapenda kueleza[...]
Sep 24, 2016BODI YA HABARI WA MWACHIA UONGOZI RAISI MAGUFURI
Bodi ya Uhuru Media Group inayosimamia vyombo vya habari vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambavy[...]
Sep 24, 2016NCHI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO VITA YA WENYEWE KWA WENYEWE IMEZUKA KANANGA
Ghasia za siku mbili katika mji wa Jamhuri ya kidemorasi ya Congo zimesababisha vifo vya watu 10.[...]
Sep 24, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.