0
MADHARA YA KUINGILIWA KINYUME CHA MAUMBILE
  1. Mwanamke anayefanyiwa mchezo huu hupata matatizo makubwa wakati wa kujifungua ikiwa ni pamoja na kutokwa na haja kubwa mfululizo wakati akijaribu kumsukuma mtoto. Tukio hili humsababishia aibu kubwa mwanamke, kiasi cha kumshushia hadhi yake mbele ya jamii.
  1. Pia anaweza kumuua mtoto kwa vile kila akimsukuma atoke, pumzi hukata kutokana na misuli inayofahamika kwa jina la ‘sphincter’ kulegea na kusababisha ambane mtoto.
  2. Umri unaposonga, haja kubwa hutoka bila kizuizi kutokana na misuli ya sphincter inayobana njia ya haja kubwa kulegea.
  3. Inaweza kusababisha saratani ya eneo hilo ‘cancer of colon’.
  4. Ugonjwa wa UTI, yaani uambukizi kwa njia ya mkojo, huwa sugu, maana akitokea mwanaume alifanya kitendo hicho kisha akafanya ngono kama kawaida, bakteria wanaoishi sehemu hiyo wanaingia na kuwa na madhara makubwa.
  5. Hasara yake kubwa mwanaume anayekufanyia mchezo huwa hawezi kukuoa, pia ni rahisi kukutangaza kwa jamaa zake na kuonekana kituko mbele za watu, kama umeolewa heshima yako hupungua ndani ya ndoa.
Mwisho kabisa baada ya kuharibiwa ni kuwa na msongo wa mawazo na kuilaumu nafsi yako. Nina imani umeona baadhi ya madhara hatari kwa mwanamke kuingiliwa kinyume cha maumbile.
 JE KUINGILIWA KINYUME NI NJIA SALAMA
MOJA, Njia ya haja kubwa haina vilainishi/lubrication asilia kama jinsi Uke ulivyo.
Hivyo wakati wa tendo la ngono husasani wakati wa uingizaji wa uume huwa inasababisha kuchubuka kwa tisu/ngozi laini ndani ya njia ya haja kubwa hiyo, na hivyo kupelekea michubuko ambayo bacteria, virusi na hata vimelea vingine kuweza kupenyea wakati wa majeraha hayo ya michubuko na hivyo kuingia katika mfumo wa damu kupitia majeraha hayo.Hii inaweza kusababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa pamoja na VVU.
Tafiti zinaonyesha ya kuwa Ngono kwa Njia ya haja kubwa ipo katika hatari kubwa ya maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa zaidi ya asilimia 30% kuliko watu wanaotumia njia ngono kwa njia ya Uke.

Vile vile mtu anakuwa katika hatari kubwa ya kupata virusi vya human papillomavirus (HPV ) ambavyo huweza kumpelekea mtu anayejihusisha na ngono kinyume na maumbile kupata muwasho katika eneo hilo la haja kubwa na hata kupelekea kupata kansa.

PILI, Tishu ndani ya njia ya haja kubwa, haijakingwa na kulindwa kwa ngozi ngumu kama ilivyo sehemu za nje za mwili. Tishu zote za nje ya miili yetu zina ngozi ambayo ni seli zilizokufa ambazo hutusaidia kutukinga dhidi ya maabukizi ya vimelea na vile vile hutulinda na vitu tofauti katika mazingira.
Hivyo ndani ya njia ya haja kubwa hakujakingwa na ulizi huo wa asili wa seli hizo ili kuweza kuhimili, hivyo kuifanya iwe katika hatari kubwa ya kusuguliwa na hivyo kuchanika ambayo hupekea kusababisha maambukizi kuwa rahisi kutokea.
Pia ngozi ndani ya njia ya haja kubwa iko tofauti na ile ya ukeni ambapo ngozi ya ukeni huweza kuhimili ile misuguano pasipo kuweza kusababisha michumbuko kwa sababu ya vilainishi asili vinavyoatikana ndian ya uke na gozi husika.

TATU, Njia ya haya kubwa ni Maalumu kupitisha Kinyesi tu.
Kwa jinsi ambavyo njia hii imeundwa ama kutengenezwa ni maalumu kwa kuhimili na kupitisha kinyeshi tu na si vinginevyo.
Njia ya haja kubwa imezungukwa na kama misuli mfano wa ringi ama kwa kitaalamu huitwa (Anal sphincter) ambayo kazi yake ni kukaza eneo hilo kabla na baada ya kujisaidia tu.
Kipindi ambapo misuli hiyo (anal sphincter)imekazwa ama kubwa kwa kuingiziwa kitu kingine kigumu huweza kusababisha maumivu makali kwa muhusika.
Panapoendelea kuwa na mrudio wa mara kwa mara wa ufanyaji wa Ngono kwa njia hii ya haja kubwa ama kinyume na maumbile hufanya misuli hiyo ya njia ya haja kubwa kuwa dhaifu ama kulegea na isiwe na uwezo tena wakukaza kama kazi yake inavyotakiwa kufanya. Na hivyo kuwa vigumu kuweza kuzuia kinyesi kuweza kupita mpaka utapokuwa tayari kuweza kukitoa hivyo kusababisha utokaji ovyo wa kinyesi.

NNE, Njia ya haja kubwa imejaa bacteria wengi.
Njia ya haja kubwa imejaa bacteria wengi sana tofauti na Ukeni kulivyo hata kama wapenzi hawana maambukizi yeyote ya zinaa au ugonjwa wowote bacteria huwa wapo tu eneo hilo na hawa ni bacteria wa kawaida (Normal flora).
Mtu anapokuwa naingiza uume ndani ya njia ya haja kuwa anakuwa anaingiza vimelea vingine vya bacteria katika eneo hilo na wanapokutana na wale bacteria wengine waliopo katika eneo hilo husababisha madhara.
Pia pale unapohamisha uume toka katika njia ya haja kubwa na kupeleka katika Njia ya Uke badi bacteria hao utawapeleka katika eneo Uke ambapo Njia ya haja kubwa inakuwa na bacteria wengi na hivyo kupelekea maambukizi ukeni na pia maambukizi katika njia mkojo.


Ngono kwa njia ya haja kubwa inaweza kusababisha madhara mengine kwa afya ya watu wanaojihusisha na Njia hii ya ngono na wanaweza kupata madhaara kama haya yafuatayo,
Pale mdomo unapogusana na njia ya haja kubwa au kugusa uume uliotoka kwenye njia ya haja kuwa kwa mdomo kunaweza kupelekea kupata kwa wote mtu na mpenzi wake kuwa katika hatari ya kupataa magonjwa ya HEPATITIS C, HERPES/ malengelenge, kupata virusi vya human papillomavirus (HPV) na maambukizo mengine.
Hata hivyo, majeraha makubwa wakati wa ngono kwa njia ya haja kubwa mara nyingine ingawa sio kila mara hali hii kutokea inaweza kupelekea Damu kuvuja kwa ndani (hemorrhoids) baada ya tendo hilo kufanyika ambalo inaweza kusababisha au kupasuka ama kuchanika kwa misuli/nyama ndani ya njia ya haya kubwa kwa sababu ya msuguano mkali na muda mwingine hupelekea kuweza kutoboka kwa utumbo mpana(colon) hii huweza kwa ni tukio la hatari zaidi ambalo huhitaji msaada wa kitabibu haraka kwa matibabu na hata kufanyiwa upasuaji zaidi na hata kupoteza maisha kunaweza kutokea.

TANO, pia kwa wanawake wengi wanaofanya ngono kinyume na maumbile wamekuwa wakipata shida wakati wa kujifungua kwa misuli yao kushindwa kuhimili kukaza kwakati wa kusukuma mtoto na hivyo inaweza kupelekea utokaji wa kinyesi wakati wa kusukuma mtoto. jambo ambalo huleta tabu kwa wahudumu wa afya kwa kutumia muda mwigi kuwahudumia.
Njia pekee ya kuepuka kabisa hatari hizo za ngono kinyume na maumbile ni kuacha kabisa ngono kwa njia hiyo ya haja kubwa.
shiriki katika ngono kwa njia ya kawaida na ikibidi kwa kutumia kondomu ili kujilinda dhidi ya kuenea kwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa.
Kuepuka kuingiza uume ndani ya uke na kisha mdomoni ikiwa uume ulikuwa umeingizwa katika njia ya haja kubwa.
Ikiwa umepata michubuko na kutoka damu baada ya ngono ama vidonda karibia na njia ya haja kubwa na hata katika maeneo ya uke basi onana na daktari wako haraka iwezekanavyo ili upatiwe tiba hii iakusaidi kuzuia maambukizi ya vimelea katika eneo la jeraha.

MADHARA ANAYOWEZA KUYAPATA MWANAUME ANAYEPENDA KUJIHUSISHA NA MCHEZO HUU WA NGONO NI KAMA IFUATAVYO;
KWANZA, Kunauwezekano wa Njia ya haja ndogo kuziba kiasi au kuziba kabisa kwa sababu ya vimelea kuingia na kuziba ama kuingia kwa kinyesi katika njia ya haja ndogo hivyo kukuweka kat

Post a Comment

 
Top