0
SEHEMU YA 1

"Maisha huwa magumu pale
unapopenda usipo pendwa,lakini
huwa
magumu zaid pale unapo kataa
kukubali kua hupendwi, daa.
Habiba
miye sikuwahi kudhania ningekuja
kugombania penzi, tena kwa mtu
ambaye hanijali siwezi kuzificha hisia
zangu lakini,sitaki kujidhalilisha pia,

huyu mwanaume mshenzi kani kana
mbele ya umati anadai hanitaki, yeye
na malaya wake walipanga kuniumiza
roho yangu najuta kwa nini niliuliza
swali lile la kumwambia achague kati
yangu na yule malaya anampenda
nani?, Ningejua ningeondoka bila
kuuliza na mimi kiherehere changu na
kukosa maarifa na kutokuuona ukweli
ndiko kumenifanya nibwatuke,, daaah.
Amakweli mtoto akililia wembe mpe
na
ndicho nilichokipata, leo hii kevi
wakunikataa mimi kwa kunidhalilisha
tena mbele za watu na mbele ya yule
malaya wake amakweli
nimeyaona,sinto
rudia tena upumbavu ule tena kwa
staili ile nimekoma nasema
nimekoma"....
..."mawazo yalikua mengi sana
mpaka nilikua nashindwa kuelewa nipo
wapi?, ghafla niliskia
"Habiba Habiba
Habiba,"
....... "nilishtuka kama mtu aliepigwa
shoti ya umeme alikua ni dada yangu
alikua ananishtua niliitikia kana
kwamba nilikua usingizini
"abeeee"
kisha nikafuta machozi "
........dada...."kunamjomba
wako hapa anakupa pole"
........" dada alikua
ananipa taarifa zile nilikua nipo mbali
sana kimawazo na wengi pale msibani
walikua wananionea huruma jinsi
nilivyokua nalia kwa maana nilikua
nalia
kupitiliza kumbe nilikua nalia kwa
mambo yangu mengine tofauti na
msiba
japo nilikua msibani na msiba ulikua
unanihusu,
......mjomba..... " pole sana habiba"..
....habiba....."akhasante
nashukuru".....
......"nilijikaza lakini
nikiwa nimekaukwa na sauti kwa ajili
ya
kulia nilipotoa asante nilifuta tena
chozi sasa sijui lilikua chozi la
kumlilia
bibi alie nitoka au kevi alie niacha,
ilikua
haieleweki, naomba bibi anisamehe
sana, huko
ulipo, maanaake ilikua kama laana
msiba mzima nilikua namuwaza kevi
kana kwamba yeye ndio alikua kafariki,
baada ya masaa kadhaa tulielekea
makaburini makaburi ya
mwananyamala kisiwani , siunajua
tena
waislamu tuliikamilisha safari ya bibi
kwa kumlaza kwenye nyumba yake ya
milele, ilikua inauma sana kwa kweli
alikua ni mtu wangu wakaribu sana
nilimzoea na siri zangu nyingi alikua
anazijua na kilichoniuma zaidi alikua
anamjua mpaka kevi nikikumbuka
hapo
machoz yananitoka zaidi. Daah!! huyu
kevi kanipa donda ambalo sito weza
kulisahau maishani mwangu, asubuhi
sana nilijihimu nakuanza kufanya
usafi
wageni walikua wengi sana jana hivyo
palikua pachafu sana nilifagia kudeki
na kuandaa chai, baadae kama mida
ya
saa nne niliingia bafuni kuoga kisha
nikajiandaa kidogo nikavaa baibui
langu baadae, nikamfuata mama
mkubwa nilikua nimeenda kuongea
nae
kuhisu mambo ya chuo, nilimuomba
ruksa, kuwa nataka niende chuo
kuangalia
majibu kama yametoka maana na
mimi
niliomba chuo cha kigamboni na
wamesema majibu yatatoka leo kwaio
nataka nikaangalie kama nimepita au
lah, mama kubwa alikua si mfuatiliaji
sana alinipa elfu kumi na kunisihi
nisichelewe kurudi, nilimkubalia,
alikua
anajua kuwa nimeomba chuo cha
kigamboni kile kilichopo n'gambo cha
mwalimu nyerere,na nikweli
ndicho.chuo nilichoomba, nilikua
naishi mwananyamala kwaio
nilichukua
gari za mwananyamala kivukoni,
nilikua
nakaa kwa kopa, basi baada kama ya
lisaa nikafika feri pantoni lilikua
linashusha sikukaa sana feri Geti
likafunguliwa tukaanza kuingia kwenye
pantoni, baada kama ya dakika ishirini
tukawa tunashuka kwenye pantoni,
nilimuona james alikua yupo getini
lakini geti la kutokea nilimfuata,naba
adae tukawa tunaongozana nilienda
nae umbali mrefu nikiwa kimya, sana
alijaribu kunidadisi lakini hakupata
jibu, nilimuongelesha mara moja tuu
pale nilipomuambia nataka niende
uwani mara moja, kwakweli sisi
wanawake tunatabu sana, nilikua
nimevaa baibui lakini nilipotoka uwani
kwenye baa flani nilikua mtu mwingine
nilikua nimevaa kimini cha ajabu
sana,nilikua spendi kutoka vile
nyumbani maana mama mkubwa
angeibua maswali na lawama, james
hakuongea kitu ila alikua anameza
mate tuu, nilijua kwa sababu alikua
ananiangalia kwa jicho la tamaa sana,
.....james...."umependeza"...
...."nilitabasamu sikumjibu
kitu chochote, moja kwa moja mpaka
kwenye gest ya entembe ilikua mitaa
ya
kwa dani karibu kidogo na kwa urasa
james alikua keshalipia teyari
alochofanya nikuchukua chips na
mayai
alivyo agiza na baadae tukaingia ndani
chumba namba 9 haikua kazi sana
nilisalula kila kitu nikabaki na chupi tu
baada ya muda alikuja
muhudumu wa gest alileta shuka na
sabuni,
james alivichukua kisha akafunga
mlango, niliamua niwe wakwanza
kuoga,nilienda kuoga na baadae
kidogo
jamesalinifuata, ikabidi tuoge wote
ilikua ni mara yangu ya kwanza
kufanya
vitu vile na james nilikua nimezoea
kuoga na kevi lakini hivi sasa hayupo
tena nilimkumbuka kiasi flani maana
yeye ndio alikua mwanaume wakwanza
kufanya nae mapenzi lakini baada ya
kuleta hitilafu mambo yakabadilika,
ilikua ngumu kidogo kumsahau kevi
lakini ilinibidi, james alikua teyari
yupo
hewani yaani alikua anamidadi ile
mbaya, alikua ananitaka kwa kipindi
kirefu lakini hakuweza kupata kitu,
sababu moyo wangu na roho yangu
Vyote vilikua kwa kevi,haikuchukua
muda
niliingia na james kitandani teyari kwa
ajili ya pambano ilikua mechi nzito
sana,lakini sikuwa na hisia hata
kidogo
nilikua namuwaza kevi tu, sura ya
james nikaitoa kabisa lakini
sikukatisha
tendo sikutaka james ajue kitu,
baadae
kama masaa matano nilijiandaa kwa
ajili ya kuondoka ilikua inabidi niwahi
nyumbani, baada kama ya nusu saa
nilifika nyumbani mida kama ya saa
kumi nambili jioni, wakati nakaribia
maeneo ya nyumbani kuna kitu
kilinishangaza kidogo, nilimkuta dada
yangu ananyonyana ndimi na bwana
Wake, nilitaka kuwapita lakini ilinibidi
nisimame kidogo kisha nigune kama
kuwashtua sikuwai kumuona jamaa
wake
pale nyumbani lakini alikua
ananiambiaga kua anaishi mitaa ya
mwanyamala hospitali, nilipo guna
walishtuka na kuachiana wakawa
wananiangalia niliogopa na
nilidondoka
chini sikuamini nilichokiona"....
Itaendeleaaa.......
Habiba kaona nini?


SEHEMU YA 2


Ilipoishia,,Habiba alikua ameaga anaenda chuo kuangalia matokeo ya walio chaguliwa kujiunga na chuo cha kumbukumbu. Ya mwalimu nyerere, huko kigamboni habiba anafanikiwa kufika kigamboni lakini sio kwa lengo lakwenda chuo bali kwenda kukutana na james, baada ya muda wanaenda gest na james wanafanya mapenzi, huku habiba akiwa bado hajalisahau penzi la kevi, wanamaliza habiba anamuaga james na safari yakurudi nyumbani kwao mwananyamala inaanza, habiba anafanikiwa kufika nyumbani lakini anamkuta dada yake akiwa nje kasimama na mwanaume wakiwa wanapigana kiss, ana washtua baada ya kumuona vizuri yule mwanaume habiba anapata mshtuko mkubwa na kudondoka, endelea nayo............" Habiba vipi" dada yangu Batuli aliniuliza kwa mshangao maanake nilipo muona bwana ake nilishindwa cha kufanya, nikaishia kudondoka, " hamna kitu" ndilo jibu nililo mpa Batuli, sikufanya kitu lakini nilikimbia kuelekea nyumbani, roho ilikua inaniuma vibaya mno yaani maafa yalikua yametawala moyoni mwangu, yaani kweli dunia chungu lakini  mbona kwangu mimi tuu, wakati nawaza yote hayo kulikua kuna begi dogo lilikua linadawa za bibi alizokua akipewa hospitali, nilizichukua kama zilivyo, kisha nikafunga mlango wangu vizuri nikazibwia zile dawa, haikua tabu sana kufanikisha zoezi la kujiua, nilikaa kama dakika mbili nikaanza kuhisi utofauti,,kufa jamani we kuskie tuu, mwili wote ulikua umechoka sijiwezi sina hali nikawa napiga kelele za kuomba msaada,,"nakufa nakufa nakufa" hakuna chochote kilichotokea nilienda kuufungua mlango ili niweze kutoka kukimbia lakini wapi, nikazidiwa nikalala pale chini yaani moyo ulikua sio wangu,,

Ghafla nikazinduka lakini sio nyumbani ilikua hospitali,, wakati sina hili wala lile nilimuona baba kwa mbali akiwa anaongea na maaskari, dada batuli alikua pembeni yangu alikua anasinzia sikutaka kumuamsha nilikua nashangaa imekuaje, nilivizia baba aje niongee nae kua hapa nimefikaje, mbona sielewi,, ghafla nikakumbuka tukio zima,, nikahisi kama mkojo unataka kunitoka, mungu wangu nilikua nataka kujiua, na ndio maana nimeletwa hapa hospitali yale madonge niliyomeza, sijui itakuaje,, baba ataniua maana nimemtoa mkoani,, alikua morogora kazini nahisi mamkubwa itakua alimpigia simu, Habiba mimi mbona mikosi inanifuata,, sikutaka hata kumshtua tena baba maana angeni gombeza sana namjua anamaneno makali sana,, nikajifanya nimelala huku nikiwa namchungulia kiwizi wizi,,basi alimalizana na yule polisi kisha akaja mpaka pale kitandani nilipo lala, alimuamsha batuli kwanza,," Batuli, Batuli Batuli" batuli aliamka "nenda kalale dereva wa bajaji yupo nje atakupeleka nyumbani niache mimi nitamuangalia dada yako", Batuli alikataa" baba we acha tu nimuangalie mimi siunajua sisi wanawake naweza kumsaidia kwenda chooni, na vitu vingine we niache mimi", Baba alipatwa na hasira kusikia vile akaanza kumfokea batuli,," wewe umeacha mpaka mdogo wako anataka kufa sasaivi unadai nikuache umuangalie, hapa ulipo unalala lala tuu, mwanangu angekufa mngenieleza nyie,, mdogo wako mpaka anakunywa sumu we ulikua wapi chanzo ni nini hujui sasa nitakuachia vipi umuangalie"  Batuli alinywea kimyaa Batuli muongeaji lakini ujanja wote ulikua mfukoni, mimi hapo naskia maneno yoote yanayotamkwa na baba, huku roho inanidunda, nikasema  nikijifanya kuamka tuu mimi maiti maana batuli kaambiwa hivi mimi je sijui itakuaje? Nikajikausha kimyaa mtoto wakike, batuli akaondoka zake nikasema mama yangu kimoyo moyo bora angebaki batuli hapa leo sijui itakuaje,, ilikua mida ya saa tatu usiku mamkubwa alikua kaja na vyakula pale hospitalini uzuri hospitali sio mbali, ni pale pale mwananyamala hospitali,, nesi aliwaambia waniamshe nile chakula, ,nilikua naskia kila kitu ila ikanibidi nizuge afadhali lakini mama mkubwa alikua kesha fika manaake ingekuaje sijui mimi na huyu mzee,," Habiba Habiba Habiba mama" ,ulikua msauti wa mzee nilijivuta nikajivuta tena kisha nikaaamka kwa utaratibu saana,," taratibu mama inuka ule" , mzee alikua ananipenda sana sema basi tu mimi mwenyewe nilikua sijatulia, hata ivyo sikuamini kama angenijali sana kiasi kile," shikamoo Baba" nilimuamkia si unajua tena ndio naamka na sijamuona siku nzima ilinibidi nizuge hivyo," marahaba Mama haya ebu kaa vizuri uanze kula sasa" niliamka nikaanza kula hakuna kitu hata kimoja nilichosemeshwa juu ya tukio nilipomaliza kula mzee alinisihi nipumzike, we acha tu nikajifanya kulala tena,,, asubuhi nililetewa juicy kubwa ya maembe na supu ya kuku,, nikawa mpaka naona aibu hivi kweli nastahili huduma hizi zote,, mzee wa watu babaangu alikua analala huku kakaa na mbu wa pale mwananyamala daa kwakweli nilimuonea huruma, , baadae nesi alikuja nakutuambia kua tumeruhusiwa chamsingi ni kuzingatia dawa na kuto mpa mgonjwa presha au stori za kumfanya akose raha,, basi mzee alinipakiza kwenye gari yake mpaka nyumbani nilikaa sebleni kidogo kisha nikaingia chumbani,  Huyu kevi jamani ananitakia nini mimi ameona haitoshi kuniacha mimi kaamua kumchukua na dada yangu batuli, huyu mbwa mwanaharamu alikua anataka kuniua, siwezi kumsamehe kamwe kwa kitendo alichonifanyia,,yule aliekua anapigana kiss na dada yangu alikua ni kevi na ndio kisa cha mimi kuanguka na kutaka kujiua amakweli mapenzi, yaskie tuu, mwanamke nimekosa raha amani yaani sielewi ulimwengu unaendaje,,lakini sikutaka mtu ajue stori ile kua nilitaka kujiua kisa kevi au kisa mapenzi, nahisi Batuli alikua anajua lakini sina uhakika sijui kevi kamwambiaje itakua kamdanganya tuu, daa nyie wanaume kweli sumu najuta kujiingiza kwenye mapenzi,, sikutaka kukaa sana chumbani ilinibidi nitoke kwenda sebuleni ili wasije kusema pengine nataka kujiua tena, ile natoka tuu namkuta james yupo sebleni na baba sijui kuna nini james hajawai kufika kwetu na hapajui sijawai kumuelekeza sasa kafikaje na nani kamleta maswali mengi nilikua najiuliza kichwani yaani nakosa majibu, ikabidi mzee aanze kuongea sasa alikua yupo batuli mama mkubwa na ndugu kama wawili ivi na james pia, " sasa bwana james mwenzako amepata matatizo kidogo sijui kama unafahamu ila ndio ametoka hospitali muda si mrefu, sijui ni nini kilimpata maana alikua amefikia hatua ya kukata tamaa na maisha, nimejaribu kumuuliza mama yake mkubwa na dada yake wakasema hawafahamu kitu ndipo polisi mmoja akatupa ushauri tuangalie simu yake mpaka anapatwa na tukio la kutaka kukatisha maisha yake wewe ndio ulikua mtu wa mwisho kuongea nae na mesej tumeziona najua nyinyi ni vijana lakini cha msingi naomba uniambie mmekwaruzana nini": wakati james anajiuma uma kujibu nilidakia haraka," hamna baba mimi kwakweli nilikua nimeenda chuo kuangalia matokeo yangu kama nimechaguliwa nilipoona sijachaguliwa ndio nikawa ninamawazo mengi rafiki zangu walikua wamechaguliwa kwakeli nilijiskia vibaya ndio maana nikachukua uamuzi ule wa kijinga," niliongopa kwa staili hiyo lakini huku moyo ukiwa unaenda mbio sana, baba ilibidi aanze kunisema " sasa mwanangu swala hilo mbona dogo sana unataka kujiua ili iweje sasa unajua utaniua mimi sasa badala ya kujiua wewe sasa, hilo sio tatizo kabisa cha msingi ungenitaarifu mimi ningejua nikusaidiaje nasio uamuzi uliouchukua, siumeomba chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere pale kigamboni"  ndio baba " nilijibu upesi huku nikiwa nanyonga nyonga vidole vyangu," mbona pale mimi najuana na watu wengi sana wewe niachie mimi, chuo hesabu umepata lakini siku nyingine usirudie sawa" aliishia hivyo."  Sawa" nilimjibu kwa haraka, watu wote wakaondokewa na hofu maana kwa kuwaangalia tuu walikua wanajua ni swala la mapenzi lakini nikawa nimeubadili mchezo kiufundi na kwa haraka zaidi kwakweli habiba mimi na huu uongo napaswa kua muigizaji,,kwa kuangalia tuu sura ya batuli alikua hajaridhika kabisa na kisingizio nilichokitoa alikua anajua nimeongopa lakini hakusema kitu na mimi sikumjali hata kidogo, basi mzee aliendelea kupiga stori pale ikawa burudani, maskini james najua anavyojiskia mkaka wa watu najua ikikua ni zaidi ya balaa kwake maswali kibao yalikua kichwani mwake  lakini ntaongea nae baadae," james, mwanangu nampenda sana lakini nikiskia umemuudhi au kumpiga itabidi udili na mimi lakini naomba umpende kama anavyokupenda mimi najua kila kitu ila cha msingi muwe makini na mkazane kwenye masomo, naskia nawewe umeomba chuo cha mwalimu nyerere" ndio" james alimjibu mzee, " vipi wewe umefanikiwa" mzee alimuuliza tena," aah nashukuru mungu nimefanikiwa" mzee alirudisha jibu" basi hongera ngoja na mimi nimtafutie huyu nafasi hapo mwalimu nyerere, ila msome sio muoane huko" mzee alimaliza kisha akaendelea nashughuli zake, sebuleni nikaachwa mimi na james tuu lakini ilikua utata kidogo maana james alikua anataka kujua mkasa mzima na mimi nilikua staki kumuambia kila kitu, nilimdanganya tu kuwa kulikua kuna kaugomvi baina ya mimi na dada yangu kwaio ndio nikaamua kutaka kujiua lakini yameisha yale sasa ivi naangalia mambo mengine, mimi kwauongo tena, yeye mwenyewe alinielewa, akaacha kuniuliza, basi nikamsindikiza ili akapande gari zakuelekea kwao, alikua anapanda gari za mwana nyamala kivukoni kwa kua alikua anakaa kigamboni, wakati namsindikiza nikakutana na Kevi barabarani nilimuangalia sana kevi, james pia aligundua kitu, aliniuliza swali kua vipi namjua yule jamaa, nilimjibu hapana" dhaa yule jamaa nikikuadisia stori yake huwezi kuamini anastori yakutisha kule kigamboni kaacha jina" wakati james ananiadisia hayo linakuja gari la mwananyamala karibu yetu likiwa tupu na james anaamua kupanda gari lile, ananiacha na maswali mengi sana nakua naumiza kichwa nasipati jibu lakini daaah mungu wangu sasa itakuaje asije kua ni muuaji yule jamaa itakua balaa mbona huyu kevi anasiri nzito sana kwakeli siwez kuvumilia ngoja nikifika nyumbani nimpigie simu james nijue alitaka kuniambia nini kuhusu kevi na anasiri gani nzito kaacha jina gani mtaani kwao? nilikua nina maswali lukuki kichwani nilienda kununua vocha ya elfu moja nikaiweka kabisa kwenye simu, ili nivizie mida ya kujirusha usiku na tigo niongee nae james kwa kina kuhisu stori ya huyo kevii nilikua nina wasiwasi kama napokea majibu ya vipimo vya ukimwi, huyu kevi itakua kafanya nini mbona sielewi, mungu si athumani saa nne ikafika nikampigia simu james, simu yake ilikua inaita tuu wala haipokelewi, baadae nikakata tamaa, ya kumpigia , saa nne kama na nusu ivi akapiga simu, alikua ananiomba samahani kwa kutopokea simu mimi sikujali nilikua nataka stori ya kevi tu basi sikuwai kumfeel james hata kidogo nilikua najua ni mcheshi mtaratibu lakini nilikua nimekufa na nimeoza kwa kevi, " sawa dia usihofu nimekuelewa usijali" nilimvuta vuta james ili anipe tuu uhondo, wa stori kuhusu kevi," vipi dia ulisema unamjua yule jamaa na ulisema kafanya vituko vipi kwani kafanya nini?" Nilidadisi kinafiki, ili nijue tuu ukweli " yule jamaa bwana anatembea na wake za watu juzi juzi kafumwa ukawa msala zaidi alafu inasemekana jamaa anamchezo wakuwapiga picha wanawake anaotembea nao nakwenda kuuza magazetini hizo picha ni zautupu na huwa ana zirusha mitandaoni"  mtumeee nimekwisha nakumbuka kevi alikua ananiambia nigeuke anipige picha na siku nyingine ananipiga picha nikiwa naoga nae na nyingine alikua ananinyoa, mungu wangu nimekwisha, wakati nawaza hayo niliendelea kumsikiliza james" duu kweli ni balaa huyo jamaa" nilisema kinafki ili stori ziendelee huku nikiwa naumia kwa kua na mimi ni muhusika pia, " Wewe unashangaa hilo mbona dogo jamaa inasemekana anasambaza ukimwi yaani kama mpo waschana watatu au wanne nyumba moja lazima atembee nao wote nawote awaambukize,"mwili wote ulikufa ganzi nikawa simsikii tena james nikakata simu nikawa nimejilaza hivi, sasa nikawa nimepata sababu nzuri yakujiua

Fuatia nini kitatokea kwa habiba itakuaje baada yakujua ukwelii.

Post a Comment

 
Top