0
Msimu wa ligi kuu England umekuwa mgumu sana kwa Cesc Fabregas  tangua uanze amecheza mechi moja tu kati ya chelsea na Liverpool napo aliingia dakika za majeruhi na kuonesha kiwango kizuri katika uwanja wa  Stamford Bridge am
bapo chelsea alipigwa 2-1, ikiwa chelsea imecheza mechi tano mpaka sasa
Kabla ya mchezo huo wa Ijumaa, alikuwa amecheza jumla ya dakika 26 na kuongeza zingine sita na sasa amefikisha jumla ya dakika 32.
Kwa aina ya mchezaji kama Fabregas ambaye alikuwa sehemu muhimu kwenye kikosi kilichotwaa ubingwa wa EPL msimu wa 2014/15, hali hii lazima imuwie vigumu sana.
Lakini bado anaonesha kuwa na moyo wa dhati wa kuendelea kutoa mchango wake klabuni hapo licha ya changamoto anazokutana nazo kwa sasa.
Amekuwa akifanya vyema pindi tu anapoingia uwanjani mfano mzuri ukiwa ni kwenye mchezo dhidi ya Watford wakati alipotoa pasi safi ya goli la ushindi wakati Chelsea ikiwa kwenye wakati mgumu.
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Fabregas aliandika hivi: “It hurts a lot to be dropping points again but we must stand up strong and learn from our mistakes.
+Thank you so much for the love.

Post a Comment

 
Top