0

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema kuwa Prof. Ibrahim Lipumba bado ni mwenyekiti halali wa Chama cha Wananchi (CUF).

Jaji Mutungi ameyasema hayo leo baada ya shauri hilo kufikishwa mezani kwake siku kadhaa zilizopita kuhusu nafasi ya uenyekiti ndani ya CUF.

Awali Prof. Lipumba ndiye alikuwa mwenyekiti, lakini alijiuzulu Agosti 2015, mwezi Agosti 2016 chama hicho kikamteua Julius Mtatiro kuwa mwenyekiti wa muda hadi hapo uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti mwingine utakapofanyika.

Lakini Prof Lipumba alirudi na kusema yeye ndiye mwenyekiti halali wa CUF kwa sababu barua yake ya kujiuzulu haikuwa imekubaliwa na Mkutano Mkuu wa CUF. 

Baada ya mvutano wa muda mrefu ndani ya chama hicho, shauri hilo lilifikishwa katika ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ambapo ametangaza rasmi kuwa Prof. Lipumba bado ni mwenyekiti.

Hapa chini ni maamuzi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

Post a Comment

 
Top