0
Mabingwa wa Tanzania bara   Dar es salaam Young Africans wanaendelea na mazoezi mjini Tukuyu, Mbeya kujiwinda na mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC itayopigwa Agosti 22 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Wakiwa huko, Yanga tayari wamecheza mechi mbili za kirafiki ambapo ya kwanza walishinda 4-1 dhidi ya Kimondo FC.
Magoli ya Wanajangwani katika mchezo huo uliopigwa uwanja wa CCM Vwawa Mbozi yalifungwa na Geofrey Mwashiuya (mawili), Simon Msuva na Amissi Tambwe.
Yanga jana imecheza mechi nyingine dhidi ya Tanzania Prisons uwanja wa Sokoine ambapo ilishinda 2-0, magoli yakifungwa na Malimi Busungu na Amissi Tambwe.
Jumapili ya wiki hii, Yanga watakabiliana na Mbeya City uwanja huo wa Sokoine.

Post a Comment

 
Top